HOME

Jun 8, 2012

HAKUNA ONGEZEKO LA MISHAHARA KWA WATUMISHI WA UMMA UGANDA!!

Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema kuwa hakutakuwa na nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma na wanasiasa wakati akilihutubia taifa jana.


Katika hotuba hiyo rais Museveni aliainisha matatizo ambayo taifa hilo linakabiliana nayo ikiwa ni pamoja na kutafuta fedha kwa ajili ya kuendeleza miundo mbinu na kuainisha kuwa nyongeza ya mishahara sio
kipaumbele.


Katika hotuba yake rais amesema nchi hiyo itakusanya fedha kwa ajili ya kujenga barabara za lami 44 ambazo zimeainishwa na UNRA kwa kuziimarisha katika mwaka ujao wa fedha.

No comments:

Post a Comment