HOME

Jun 11, 2012

KENYA KATIKA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO!!

Prof George Saitoti enzi za uhai wake
Kenya imetangaza siku tatu za maombolezo baada ya kifo cha Waziri wa Usalama wa Kenya, Prof. George Saitoti na naibu wake, Orwa Ojode, kwenye ajali ya helikopta ya polisi katika eneo la Ngong, nje ya Nairobi.

Ajali ya helikopta iliyochukua maisha ya wakenya sita akiwemo waziri wa usalama wa ndani wa Kenya Prof. George Saitoti na naibu wake Orwa Ojode jana asubuhi.
 
Wakati huo huo rais Mwai Kibaki wa Kenya leo asubuhi ameongoza kikao cha baraza la mawaziri kujadili vifo hivyo.


Sababu ya ajali hiyo haijafahamika ingawa mashuhuda wamekuwa wakielezea jinsi walivyoiona helikopta hiyo ikitoa moshi na kupotea uelekeo.

No comments:

Post a Comment