HOME

Jun 6, 2012

BOMU LA KUJITOA MHANGA LAUA 21 AFGHAN!!

Polisi nchini Afghan imeviambia vyombo vya habari kuwa bomu la kujitoa mhanga limeua watu 21 katika shambulio lililofanyika katika hoteli karibu na mji wa Kandahar.


Mkuu wa polisi wa jimbo hilo Abdul Raziq amesema madereva wanaowahudumia majeshi ya NATO walikuwa wanakusanyika katika hoteli hiyo wakati wa shambulio hilo.


Taarifa hiyo ya jeshi la polisi inasema watu 22 walijeruhiwa kufuatia shambulio hilo karibu na uwanja wa ndege wa mji huo.

No comments:

Post a Comment