HOME

May 30, 2012

COUNTING OF VOTES FOR EALA POLLS UNDERWAY!!

Casting of ballots for Uganda’s representatives to the regional Parliament has ended and counting of ballots is underway.

The Speaker of Parliament Rebecca Kadaga is presiding over the counting as a clerk reads out the names for tallying. 

Earlier, the Leader of Opposition in Parliament Nathan Nandala Mafabi exerted his authority and suspended UPC and DP from all Parliament opposition activities.

Nandala told the House that both parties defied the opposition position to boycott EALA elections until the Arusha Court ruling is enforced.  

MWANAMKE ANAEDAI KUZAA NA MBUNGE,ADAI MILIONI 1.2 KSH ZA MATUNZO YA MTOTO!!

Mbunge wa jimbo la Mwea Peter Gitau
Mwanamke raia wa Kenya anaedai kuwa ana mtoto wa miezi miwili aliyezaa na mbunge amedai shilingi za Kenya milioni 1.2 kutoka kwa mbunge huyo kwa ajili ya matunzo ya mtoto.

Hata hivyo  mbunge huyo wa jimbo la Mwea Bw. Peter Gitau amekana madai hayo akisema ameoa na ana familia yenye furaha.

Katika kesi hiyo iliyofunguliwa katika mahakama jijini Nairobi mwanamama huyo mwenye umri wa 21 anayefanya kazi katika kampuni binafsi amedai kuwa mbunge Gitau alimpa ujauzito na kisha kumtelekeza.

Ameendelea kudai kuwa mbunge huyo alimuahidi kumpatia kazi, gari na nyumba iwapo atamzalia mtoto.

TAYLOR AHUKUMIWA MIAKA 50 JELA!!

Rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor leo amehukumiwa kifungo cha miaka 50 jela baada ya mwezi uliopita kutiwa hatiani kwa makosa ya uhalifu wa kivita na mahakama maalumu ya Umoja wa Mataifa huko The Hague hukumu iliyotolewa na Jaji Richard Lussick.

Waendesha mashtaka wa mahakama maalumu ya Sierra Leone waliitaka mahakama hiyo kumfunga mtuhumiwa huyo miaka 80 jela ambapo upande wa utetezi ulidai kuwa adhabu hiyo ni kubwa mno.

Taylor amesisitiza kuwa hana hatia na anatarajia kukata rufaa kupinga adhabu hiyo na mchakato wa rufaa unaweza kuchukua zaidi ya miezi sita.

Mahakama hiyo ilimtia hatiani Taylor kwa mashitaka 11 yanayohusiana na uhalifu wa kivita, ubakaji na mauaji.

May 28, 2012

WATU KADHAA WAJERUHIWA KATIKA MLIPUKO NCHINI KENYA!!

Majeruhi wakiingizwa kwenye gari la wagonjwa kukimbizwa hospitali
Watu kadhaa wamejeruhiwa nchini Kenya katika mlipuko ambao umetokea katika jumba la maonyesho karibu na jengo la Chuo Kikuu cha Mlima Kenya pembezoni mwa eneo lenye shughuli nyingi Moi.

Mlipuko huo ambao chanzo chake hakijajulikana mpaka sasa umetokea majira ya saa saba na robo mchana na kutingisha majengo yanayozunguka eneo hilo.

Jengo hilo linalojulikana kama  Assanands lilishika moto punde mlipuko huo ulivyotokea lakini vikosi vya zimamoto vimefanikiwa kuzima moto huo ambao umeunguza sehemu ya jengo.

Imeripotiwa kuwa bado kuna watu wamekwama ndani ya jengo ambalo ndani kuna maduka ya nguo.