HOME

May 27, 2013

SHUHUDIA WILL SMITH AKIPIGA PENALTY KWENYE SHEREHE ZA FAINALI YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

Kuelekea fainali ya UEFA Champions League iliyopigwa juzi na Bayern Munich kuukwaa uchampion wa Ulaya, staa wa Hollywood Will Smith na mwanae Jaden Smith walipata nafasi ya kushiriki the Ultimate Champions Match ambayo pia ilishirikisha wakali wa zamani kama Luis Figo, Gianfranco Zola na Robert Pires.


Isivyotegemewa na wengi, baba na mwana Smith walijikuta wakiiba show nzima kutokana na vimbwanga vyao katika uchezaji mpira hasa penalty.

Kati ya penalty KUMI walizopiga, walifanikiwa kumfunga goli moja tu, Edwin Van De Sar aliyekuwepo golini, baada ya Will Smith kuamua kumzuia asidake penalty hiyo.

Fuatilia video ya tukio hilo kwa ufupi hapa chini.

KUTANA NA WAWAKILISHI WA TANZANIA KATIKA JUMBA LA BIG BROTHER AFRICA SEASON 8 - THE CHASE


FEZA KESSY 
Soma wasifu wake wa BBA8 HAPA


AMMY NANDO
Soma wasifu wake wa BBA8 HAPA

BAADHI YA PICHA ZA AJALI YA TRENI NA GARI AINA YA RAV 4 UKONGA ASUBUHI HII.




Taarifa zinasema kwamba kuna ajali imetokea leo asubuhi maeneo ya Ukonga, ambayo imehusisha treni na gari aina ya RAV 4 ambayo ndani ilikuwa na watu wawili. Dereva wa RAV 4 amekufa papo hapo na abiria ambaye ni mwanamke hali yake ni mbaya yupo mahututi hospitali!

Picha kwa hisani ya MPEKUZI BLOG.

NEYMAR KUJIUNGA NA BARCA MWEZI JULAI.


Staa wa Brazil na klabu ya Santos Neymar da Silva Santos Jr, hatimaye amekubali kujiunga na klabu yenye mafanikio makubwa ya Hispania, Barcelona. Ripoti zinaonesha kuwa Neymar, ataichezea klabu hiyo kuanzia Julai mwaka huu, mara baada ya kumalizika kwa kombe la mabara. Neymar amejitia kitanzi cha miaka mitano kwa miamba hiyo ya Ulaya yenye wakali kama Lionel Messi, Xavi Hernandez, Andre Iniesta na Pedro Rodriguez.

Hapa chini ni official Twitter handle ya Barca, ilipo-confirm habari hizi.