HOME

Apr 4, 2012

WATU SABA WAMEKUFA KATIKA MLIPUKO NCHINI SOMALIA!!

Watu saba wamekufa mapema leo kufuatia mlipuko mkubwa katika ukumbi mpya wa kitaifa uliofunguliwa hivi karibuni uliopo jijini Mogadishu nchini Somalia.


Mlipuko huo umetokea wakati wa hafla ya kuamdhimisha mwaka mmoja tangu televisheni ya taifa kuanza kuyapeperusha matangazo yake.


Takriban watu saba wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa, wakiwemo wabunge ambapo Waziri Mkuu Abdiweli Mohamed Ali alikuwepo kwenye hafla hiyo lakini haijabainika ikiwa alijeruhiwa.


Mshambuliaji wa kike wa kujitoa mhanga ameripotiwa kufanya shambulio hilo.

SOKO LA SAMAKI FERI LILIPOWAKA MOTO LEO ASUBUHI!!

Picha zote na Hassan Mabuye
Soko la feri upande wa kukaangia samaki limeshika moto leo tarehe 4/4/2012 asubuhi katika muda wa saa nne (4) mpaka sita (6) nakulazimu gari la zima moto yaani fire kuja kuuzima moto huo ambao ulikuwa unaendelea kuzimwa na wananci wengi ambao  ni wachuuzi wa samaki sokoni hapo.


Hata hivyo haikujulikana ni hasara kiasi gani imesababishwa na moto huo na hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa katikla tukio hilo.



MWANAMKE MZEE AWEZA KUIDHIBITI NDEGE BAADA YA MUME WAKE RUBANI KUZIMIA NA KUFA!!


Ndege iliyodhibitiwa na Bi. Collins isiweze kutua ghafla
 Mwanamke mzee raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 80 ambaye alikuwa na ufahamu kidogo wa kurusha ndege aliweza kuidhibiti ndege na kufanikiwa kutua kwa dharura huko Wisconsin baada ya mumewe rubani kuzimia na kufa.


Bibi huyo ambaye ametambulika kwa jina la Helen Collins alikuwa mtulivu wakati akishusha ndege hiyo ndogo aina ya Cessna na kutua katika uwanja wa ndege wa Cherryland pamoja na kwamba alijua mume wake amefariki.


Mwanae James Collins ambaye naye ni rubani aliyefuzu alimuongoza mama yake kwa njia ya radio na kufanikiwa kutua amesema mama yake aliwahi kufanya masomo ya msingi ya urubani ya kuruka na kutua miaka 30 iliyopita.