
Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa upinzani kupitia kwa kiongozi wa kambi hiyo Mhe. Freeman Mbowe kuomba mwongozo wa spika leo bungeni mjini Dododma kuhusiana na hatua hiyo iliyochukuliwa na naibu spika wa bunge Job Ndugai ambayo amesema imezua maswali miongoni mwa wabunge.
Spika Makinda amewata wabunge kuwa watulivu na kuacha malumbano kwani atatoa ufafanuzi wa jambo hilo katika vikao vya jioni vya bunge.
Wabunge waliokumbana na kadhia hiyo ya kutolewa nje ya ukumbi wa bunge ni Mbunge wa Nyamagana Hezekiah Wenje, Highness Kiwia wa Ilemela, Joseph Mbilinyi wa Mbeya Mjini, Godbless Lema wa Arusha mjini na Mchungaji Peter Msigwa wa Iringa Mjini ambapo chanzo cha kufukuzwa kwao kimedaiwa ni kuwazuia askari wa bunge kumtoa nje Lissu ambaye alikuwa ameamriwa kutoka nje na naibu Spika baada ya kuingia hotuba ya Mwigulu Nchemba mbunge wa Iramba Mashariki.
No comments:
Post a Comment