
Tangu mwaka 2000 kiwango cha vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Malaria kimepungua kwa asilimia 25%. Kuna nchi 50 kati ya nchi 99 zinazoendelea kufanya vyema ili kufikia Malengo ya Maendeleo ya Millenia kwa mwaka 2015 kwa kupunguza vifo kwa asilimia 75%.

Zaidi ya watu millioni 200 wanashambuliwa na ugonjwa wa Malaria. Kesi nyingi hazipimwi wala kupatiwa tiba muafaka. Dawa zisizo na viwango zinasababisha usugu, jambo ambalo linaweza kukwamisha jitihada za Jumuiya ya Kimataifa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria.
Kauli mbiu inayoongoza Maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani kwa Mwaka 2013; Wekeza kwa siku za baadaye. Shinda Malaria.
Credits: WHO, unmultimedia and AP
No comments:
Post a Comment