
Wafanyakazi wa uokoaji wanafanya kazi kwa nguvu zote na watu wa kujitolea wakitumia vifaa na mikono kutafuta kuwaokoa waliosalimika kutokana na jengo hilo kuanguka.
Makumi kwa maelfu ya familia zilizopoteza ndugu zao walionekana katika eneo hilo wakiwalilia ndugu zao waliopoteza maisha.

Matukio ya majengo kuporomoka nchini Bangladesh ni ya kawaida kutokana na majengo mengi marefu kujengwa kinyume na sheria za ujenzi.
Serikali ya nchi hiyo imetangaza siku moja ya maombolezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoto kuwakumbuka waliopoteza maisha kufutia tukio hilo.
Picha: Reuters
No comments:
Post a Comment