
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mjumbe wa kamati ya utendaji ya TABOA Rajab Kassim amesema kwa sasa kero hiyo imepungua kwa zaidi ya asilimia 80 kufuatia kampeni ya kuwaondoa wapiga debe katika eneo hilo.
Amesema kampeni hiyo ilifanywa na Taboa pamoja na halmashauri ya jiji kwa kipindi cha wiki mbili hadi sasa inayowashirikisha pia polisi na askari wa ulinzi shirikishi waliopo chini ya chama hicho ambayo kwa kiasi kikubwa imefanikiwa kuwaondoa wapiga debe hao.
No comments:
Post a Comment