HOME

Jun 6, 2012

VIPAUMBELE VYA KAMBI YA UPINZANI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013

Mwaka 2011/2012 Kambi ya Upinzani Bungeni ilitangaza Vipaumbele vyake katika Bajeti Mbadala ambavyo vilikuwa:
1.    Kupunguza misamaha ya kodi mpaka 1% ya pato la Taifa kutoka 3%


2.    Kupunguza kodi kwenye bidhaa za mafuta ya petrol na dizeli ili kupunguza mfumuko wa bei
3.    Kufuta mfumo wa posho za vikao (Sitting allowances).
4.     Kupeleka sehemu ya tozo ya ujuzi (Skills Development levy-SDL) kwenye bodi ya mikopo ya  elimu ya juu.
Masuala haya pamoja na mengine yalikuwa sehemu ya Bajeti kivuli iliyowasilishwa Bungeni na Kambi ya Upinzani.
Mapendekezo mawili,
(1) Kodi za mafuta ya Petrol na Diseli na
(2) Tozo ya SDL yalikubaliwa na kutekelezwa. Pendekezo la misamaha ya kodi lilikubaliwa  lakini Serikali imeshindwa kulitekeleza na pendekezo la kufutilia mbali posho za vikao halikukubaliwa.
Kambi Rasmi ya Upinzani inataka maelezo ya kina ya kwa nini Serikali imeshindwa kutekeleza ahadi yake iliyoitoa Bungeni kwamba misamaha ya kodi itapungizwa mpaka kufikia 1% ya pato la Taifa. Halikadhalika Kambi ya Upinzani inarejea wito wake wa
kufutwa kwa Mfumo wa posho za vikao (sitting allowances).

Serikali imependekeza Bajeti ya Tshs. 15trillioni kutoka Tshs. 13 trillion. Hata hivyo ni dhahiri kwamba Bajeti ya 2011/12 ilikuwa ina changamoto kubwa za utekelezaji. Serikali ieleze itawezaje kutekeleza Bajeti ya 15trillioni?
Katika Bajeti Mbadala ya 2012/2013 Kambi ya Upinzani itajikita katika maeneo yafuatayo na kuishinikiza Serikali kuyatekeleza.
1. Kuendelea kushinikiza kupunguzwa kwa misamaha ya kodi mpaka 1% ya Pato la Taifa.
Hivi sasa misamaha ya kodi ni sawa na misaada yote kutoka nchi wahisani, Tshs 1.03 trillioni ni sawa na 3% ya Pato la Taifa.
2. Kuelekeza raslimali fedha kwenye maendeleo vijijini hasa kujenga miundombinu kama barabara za vijijini na umeme vijijini.
3. Kuelekeza fedha za kutosha  kukarabati Reli ya Kati na kufufua njia za Reli za Tanga, Moshi na Arusha.
4. Kuongeza wigo wa kutoza  tozo la ujuzi (Skills Development Levy) ambapo sasa waajiri wote walipe ikiwemo Serikali na mashirika ya umma. Pia kupunguza tozo hili mpaka 4% ambapo 1/3 itaenda VETA na vyuo vya Ufundi na 2/3 itaenda Bodi ya Mikopo
ili kukabili changamoto ya mikopo kwa wanafunzi.
5. Kushusha kima cha chini cha kodi ya mapato (PAYE) mpaka 9% ili kuwezesha wananchi wa hali ya chini kubaki na fedha za kutumia na kukuza uchumi.
6. Kuongeza mapato ya ndani na kupunguza mikopo ya kibiashara kwa kuhakikisha mapato ya ndani yanafikia 20% ya pato la taifa, kuongeza nguvu za kisheria na udhibiti ili TRA ikusanye mapato zaidi kwenye kampuni za simu na kwenye shughuli za uchimbaji wa
madini, mafuta na gesi.
7. Kutayarisha Taifa kuwa na uchumi wa Gesi.
8. Kupunguza /kufuta kodi kwenye bidhaaa za vyakula kwa muda maalum ili kushusha mfumuko wa bei.
9. Kuweka mfumo mpya wa elimu kwa kushirikisha sekta binafsi katika kutoa elimu kwa ubora zaidi, ikiwemo kuundwa kwa chombo cha Udhibiti wa Elimu(Regulatory authority)
10. Kutoa vipaumbele na unafuu vya kikodi kwa viwanda vya ndani vinavyotumia malighafi za nchni hasa za kilimo na zenye kuongeza ajira kama Korosho,Pamba na Mkonge.
Kambi ya Upinzani itaendelea kufuatilia kwa karibu sana suala la kukua kwa deni la Taifa amabalo limefikia hadi Tshs 22 trillioni na kutaka ukaguzi maalum kuhusu akaunti ya Deni la Taifa.
Kambi ya Upinzani itawekeza kusimamia kwa karibu suala la matumizi yasiyo na tija ya Serikali hasa kwenye  magari na posho mbalimbali na Kwamba  fedha nyingi zitumike kwa miradi  mikubwa ya maendeleo ili kukuza ajira. Halikadhalika namna ya kupta fedha za kutekeleza mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano


Asanteni sana!
…………………………….
Zuberi Kabwe Zitto(Mb)
Waziri Kivuli-Fedha na Uchumi.

FIRST LADY,PATIENCE JONATHAN RESPONDS TO ALLEGATIONS OF BEING RESPONSIBLE FOR DANA PLANE CRASH!!

The First Lady of Nigeria, Patience Jonathan came under criticism yesterday as news of the alleged closure of the nation’s airspace for a Presidential jet conveying her to Lagos on Sunday went viral on BlackBerry Messenger and online social networks.


The closure was said to have prevented the pilot of the distressed Dana Air’s plane from making an emergency landing at the airport. Reports circulated claimed that although the Dana plane had an engine failure, the distressed aircraft could have made it to the airport if it was not delayed by the VIP movement.


However, in response to this, the Special Assistant (Media) to the Minister of Aviation, Mr. Joe Obi, said the airspace was never closed for the First Lady on Sunday. He noted that the First Lady arrived in Lagos at about 4.45pm on Saturday, 2nd June, 2012 and only departed for Abuja on Monday, the 4th of June, 2012 at 1.30pm, whereas the ill-fated Dana flight 0992 departed Abuja on Sunday, 3rd of June, 2012 at 2.54pm and its last contact with the Lagos Control Tower was at 3.42pm as has already been announced.


The rumours prompted a response from the Office of the First Lady:


I am responding to the rumor mongers because of the involvement of the script writers of those that wish to heat up the polity of Nigeria at every event or given opportunity. Like they have always done, using every opportunity to make Nigeria ungovernable. Why would a group of people in different disguises want to play politics with this sad event just to get back to political rivals or superiors?


This morning, reports from one Ade Atobatele….Information Technology and Services has filtered the air. Don’t know which of the firms that is, claimed that the Dana Airline misfortune was caused by the closure of airspace for the first lady’s aircraft. He was quoted as saying he was informed by a pilot of a private Jet that also had to hover in the air for 2 hours 15mins before the airspace opened for landing. He has conned his story that the social, electronic and print media has started reporting it without verifying his source.

Jun 5, 2012

MBUNGE ALIYEFIKISHWA MAHAKAMANI KWA RUSHWA!!



Pichani Mbunge wa jimbo la Bahi Tanzania, Bw. Omar Ahmed Badwel akiwa anafikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za rushwa.
  
Mbunge wa jimbo la Bahi nchini Tanzania, Bw. Omar Ahmed Badwel amepandishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, akikabiliwa na mashtaka mawili ya kudai na kupokea rushwa.

Katika shitaka la kwanza, imedaiwa kuwa kati ya Mei 30 na Juni 2 mwaka huu, mtuhumiwa aliomba rushwa ya shilingi milioni nane kutoka kwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mkuranga, Bi. Sipora Liana ili ashawishi kamati yake ipokee na kukubali ripoti ya hesabu za halmashauri hiyo.

Imedaiwa pia kuwa kipindi hicho hicho, mtuhumiwa amekamatwa akipokea rushwa ya shilingi za milioni moja za Tanzania, kutoka kwa Bi. Sipora kwa lengo lilelile la kushawishi kamati yake ipokee na kupitisha hesabu za halmashauri ya wilaya ya Mkuranga.

Jun 4, 2012

AJALI YAUA WATU 150 NIGERIA!!

Siku tatu za maombolezo ya kitaifa zimetangazwa kuanzia leo nchini Nigeria kufuatia ajali ya ndege ambapo zaidi ya 150 walikufa.


Ndege hiyo aina ya Boeing MD-83 iliangukia eneo moja la kuchapisha karatasi na makaazi mjini Lagos kabla ya kulipuka. Makundi ya wokozi yamekuwa eneo la ajali usiku kucha.


Taarifa zinasema abiria wote katika ndege hiyo walikufa. Hakuna majeruhi katika eneo la ajali japo haijabainika rasmi ni watu wangapi ambao wamekufa.


Ndege hiyo inamilikiwa na kampuni ya Dana Air ambayo hutoa huduma zake kati ya mji wa Abuja na Lagos. Ajali hiyo ilitokea katika mji wa Iju Kaskazini mwa uwanja wa ndege.